Jumanne, 30 Agosti 2016

Crazy GK ageukia kwenye muziki wakuimba

Msanii wa Kundi la East Coast, King Crazy GK ameamua kuingia studio na kuandaa wimbo wa kuimba

Rapper huyo amesema kuwa ushindani uliopo kwenye game la muziki ni tofauti na zamani hali ambayo imemfanya abadilike.
“Nimeamua kuimba lakini ni kutokana na game la Tanzania kubadilika,” GK alikiambia kipindi cha Enewz cha EATV. “Zamani tulikuwa tukishindana sisi wa Tanzania kama Juma Nature, AY na wengine lakini kwa sasa muziki wa bongo ume’change’ na kuingia mpaka wakina Wizkind, so kubadilika muhimu”
GK amesema ujio wake mpya utaweza kuleta ushindani na kumuweka sehemu nzuri katika muziki wa Tanzania pamoja na kimataifa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni